Maahadi ya Quráni tawi la wanawake inatangaza (mashindano ya Nuur ya kwanza) ya kuandika kitabu kuhusu maarifa ya Quráni

Maoni katika picha
Maahadi ya Quráni tukufu tawi la wanawake chini ya kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinaadamu katika Atabatu Abbasiyya imetanga kufanya (shindano la Nuur la kwanza) linalo husu wanawake peke yake, la kuandika vitabu kuhusu maarifa ya Quráni, ili kukienzi kitabu cha Mwenyezi Mungu na kufichua hazina zake pamoja na kutumia muda vizuri katika kipindi hiki ambacho dunia inapitia kwa sasa.

Mkuu wa Maahadi Ustadhat Manaar Jawadi Jiburi ameuambia mtandao wa Alkafeel kuwa: “Shindano hili ni sehemu ya harakati zilizo zoweleka kufanywa na Maahadi, kwa ajili ya kuongeza kiwango cha kushikamana na utamaduni wa Quráni kwa wanawake”.

Akabainisha kuwa: “masharti ya kujiunga na mashindano ni haya yafuatayo:

  • - Mashindano haya ni maalum kwa ajili ya wanawake tu.
  • - Maudhui za kitabu zihusu Quráni tukufu, sura na aya zake pamoja na matamshi yake.
  • - Kitabu kisiwe na mlengo wa kujenga chuki na ugonvi.
  • - Kitabu kisiwe kimesha wahi kuandikwa au kutolewa na watu wengine.
  • - Kiandikwe kwa hati ya (simplified Arabic) kwenye karatasi ya (A4), kurasa zake ziwekwe namba na kiwe na maneno yasiyopungua (5000) na yasiyozidi (15000)”.

Akaongeza kuwa: “Vitabu vyote vitawasilishwa kwenye kamati ya majaji, mwisho wa kupokea vitabu hivyo ni tarehe (1 Oktoba 2020m).

Kuna zawadi kwa washindi watatu wa kwanza ambazo ni:

Mshindi wa kwanza: 150,000 dinari za Iraq.

Mshindi wa pili: 100,000 dinari za Iraq.

Mshindi wa tatu: 75,000 dinari za Iraq.

Pamoja na zawadi zingine zitakazo gawiwa kwa washindi kumi wa mwanzo”.

Akasema: “Washiriki wapeleke kazi zao moja kwa moja kwenye ofisi za Maahadi ya Quráni tukufu kitengo cha wanawake mjini Najafu/ mtaa wa Hanana, au kwenye matawi yake yaliyopo mikoani, aidha wanaweza kutuma kwa barua pepe ifuatayo nafhat296@gmail.com”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: