Kituo cha habari Alqamar kimetangaza ratiba yake katika mwezi wa Muharam

Maoni katika picha
Kutokana na kukaribia mwezi wa Muharam wa mwaka 1442h, kituo cha habari Alqamar chini ya Maahadi ya Turathi za Mitume katika Atabatu Abbasiyya tukufu, kitakuwa na ratiba maalum ya kuomboleza mwezi wa huzuni kupitia mitandao yake ya mawasiliano ya kijamii.

Shekh Hussein Turabi mkuu wa Maahadi amesema kuwa: Ratiba iliyo andaliwa inaendana na utukufu wa mwezi huo kwa siku zote tena kwa kufuata nyakati maalum, miongoni mwa vipengele vya ratiba hiyo ni:

  • Hurufu Twafu: Ratiba ya mihadhara inayo elezea harakati ya Husseiniyya.
  • Duraru-Mimbari: Vipande vya video za mihadhara ya Shekh Ahmadi Waailiy.
  • Shairi kutoka Twafu: Ratiba ya mashairi ya tukio la Twafu.
  • Matukio ya Muharam: Kuangazia mambo yaliyo tokea katika mwezi wa Muharam na Safar.
  • Pamoja na wafuasi wa Hussein (a.s): Kuangazia historia ya wafuasi wa Imamu Hussein (a.s).
  • Athari za kijamii kuhusu harakati za Imamu Hussein (a.s) na jinsi zinavyo athiri familia na jamii.
  • Walisema kuhusu Hussein (a.s): Ratiba inayo angazia swala la Husseiniyya katika mtazamo wa Mustashriqina.
  • Visa vya wanachuoni: Ratiba ya kuangalia yaliyotokea kwa wanachuoni kuhusu swala la Husseiniyya.

Fuatilia ratiba hiyo kupitia mitandao ifuatayo:

Facebook

Yotube

Telegram

instagram
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: