Majengo la Shekh Kuleini yamekamilisha maandalizi ya kupokea mazuwaru wa ziara ya Arubaini

Maoni katika picha
Sayyid Ali Mahdi Swafi kiongozi wa majengo ya Shekh Kuleini yaliyo chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu katika barabara ya (Bagdad – Karbala), amesema kuwa wamekamilisha maandalizi ya kupokea mazuwaru wa Arubaini katika sekta zote za utowaji wa huduma za chukula mazali na afya.

Akaongeza kuwa: “Tulianza mapema kujiandaa kwa ajili ya ziara hii, maandalizi yamehusisha vitu vingi, miongoni mwa vitu hivyo ni:

  • - Kuandaa kumbi maalum za kupokelea mazuwaru.
  • - Kupuliza dawa za kujikinga na maambukizi kwenye majengo.
  • - Kuandaa jiko na kuweka aina zote za chakula kinacho hitajika.
  • - Kufanya ukarabati vifaa vya umeme.
  • - Kufanya ukarabati wa vyoo na kuweka mahitaji yote muhimu na vifaa vya usafi.
  • - Kuandaa mabango ya vituo vya afya kwa kushirikiana na idara ya afya ya mkoa wa Karbala upande wa wanaume na wanawake.
  • - Kuandaa sehemu maalum za kusaidia watu waliopotea au kupotelewa.
  • - Kuweka utaratibu wa kutoa maelekezo kwa mazuwaru chini ya muongozo wa idara ya afya.
  • - Kuandaa kundi la watu wa kujitolea watakao saidiana na watumishi wa majengo ya Shekh Kuleini katika kutoa huduma mbalimbali.
  • - Kuandaa kikosi cha huduma ya kwanza na uokozi pamoja na gari la wagonjwa kwa ajili ya kupambana na tatizo lolote linaloweza kutokea Allah atuepushie”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: