Kwa washiriki (125): yametangazwa majina ya washindi wa shindano la (Khalaful-ula min khairul-wara)

Maoni katika picha
Idara ya Quráni tawi la wanawake chini ya ofisi ya maelekezo ya dini katika Atabatu Abbasiyya tukufu, imetangaza majina ya washindi wa shindano la (Khalaful-ula min khairul-wara) lililofanywa katika kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Imamu Hassan Askariy (a.s) na kupata ushiriki wa watu (125).

Kiongozi wa idara bibi Fatuma Sayyid Abbasi Mussawi ameuambia mtandao wa Alkafeel kuwa: “Shindano limepata muitikio mkubwa, washiriki wametoka mikoa tofauti, kila mshiriki alitakiwa kusoma kitabu chenye kurasa (200) kwa ajili ya kuingia kwenye shindano”.

Akabainisha kuwa: “Lengo kuu la shindano hili ni kuangazia historia ya Maasumina (a.s) na yaliyotokea katika uhai wake na kuongeza maarifa ya kuwatambua Ahlulbait (a.s)”.

Akamaliza kwa kusema: “Aidha idara ya Quráni inatoa shukrani ya dhati kwa wakina dada wote walioshiriki na tunawaombea mafanikio mema, pongezi za pekee ziwafikie wakina dada wote baada ya kupata ushindi mkubwa”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: