Muitikio mkubwa wa wanafunzi waliokubaliwa kujiunga na chuo cha Alkafeel

Maoni katika picha
Chuo kikuu cha Alkafeel chini ya kamati ya malezi na elimu ya juu katika Atabatu Abbasiyya tukufu kimeanza kupokea wanafunzi waliokubaliwa katika vitivo vyake kwa mwaka wa masomo (20 – 2021), kwa lengo la kuthibitisha nafasi zao katika vitivo vya: (Udaktari wa meno, famasia, teknolojia ya matibabu na afya/ kitengo cha teknolojia za maabara, teknolojia ya uhandisi/ kitengo cha teknolojia za kihandisi na kompyuta, sheria), kufuatia kuanza msimu wa masomo ya vyuo binafsi chini ya utaratibu wa wizara ya elimu ya juu na utafiti wa elimu hatua ya nne na ya mwisho, nayo ndio hatua ya usajili.

Makamo rais wa chuo Dokta Nawaal Almayali amesema kuwa: “Chuo kimesha kamilisha maandalizi yote, ya kupokea wanafunzi waliokubaliwa katika ofisi za chuo zilizopo Najafu/ mtaa wa Nidaa nguzo namba 23/ jirani na jengo la makazi Amiraat”.

Akasisitiza kuwa: “Wanafunzi wanatakiwa kuja na vielelezo vinavyo hitajika ambavyo ni:

  • 1- Kitambulisho cha uraia au cheti cha kuzaliwa (nakala halisi na kopi 1).
  • 2- Kitambulisho cha uraia au cheti cha kuzaliwa cha mzazi (nakala halisi na kopi 1).
  • 3- Kitambulisho cha makazi (nakala halisi na kopi 1).
  • 4- Cheti cha kuhitimu elimu ya sekondari (uthibitisho).
  • 5- Kodi ya kukubaliwa kwake.
  • 6- Picha binafsi ndogo (6).
  • 7- Cheti cha daktari (kutoka kituo cha afya katika mji anaoishi mwanafunzi).
  • 8- Ada ya masomo”.

Akamaliza kwa kusema: “Kitengo cha usajili kinafanya kazi siku zote za wiki ispokua Ijumaa, kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: