Kufuatia kumbukumbu ya kuzaliwa kwa bibi Zaharaa (a.s) idara ya Quráni inafanya shindano la (Fatuma Zaharaa furaha ya Mtume)

Maoni katika picha
Idara ya Quráni chini ya ofisi ya maelekezo ya dini kitengo cha wanawake kinacho fungamana na ofisi ya katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya inafanya shindano la (Fatuma Zaharaa –a.s- furaha ya Mtume), kufuatia kumbukumbu ya kuzaliwa kwa bibi Zaharaa (a.s) mwezi 20 Jamadal-Aakhar.

Kiongozi wa idara Ustadhat Fatuma Sayyid Abbasi Mussawi amesema kuwa: “Kutokana na kujali turathi za maasumina katika Ahlulbait (a.s) tumeamua kufanya shindano hili katika kuadhimisha kuzaliwa kwa mbora wa wanawake wa duniani Fatuma Zaharaa (a.s)”.

Akaongeza kuwa: “Shindano linahusu kuandika muhtasasi wa kitabu cha (Mushahadaat mala-ul Al-Aála sherehe ya hadithul-Kisaa) cha Sayyid Muhammad Ali Halo, mihtasari hizo zitawasilishwa kwenye jopo la majaji”.

Akasema: “Mashariti ya kushiriki ni:

  • 1- Umri wa mshiriki usiwe chini ya miaka 18.
  • 2- Mihtasari utumwe kupitia barua pepe ya idara ya Quráni”.

Akaendelea kusema: “Shindano la wanawake tu, na mwisho wa kupokea mihtasari ni tarehe (31/1), usizidi kurasa (10) na itakayo zidi haitafanyiwa kazi”.

Akakumbusha kuwa: (Majina ya washindi yatatangazwa kupitia mtandao wa kimataifa Alkafeel baada ya kumaliza shindano, pamoja na ukurasa wa idara ya Quráni wa Facebook”.

Kwa maelezo zaidi fungua link hii
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: