Marjaa Dini mkuu amesisitiza mamlaka zenye maambuzi hususan viongozi wakuu watumie zaidi akili na sio lugha chafu.
Hayo yamesemwa wakati Mheshimiwa Ayatullahi mkuu Sayyid Ali Hussein Sistani alipokutana na Papa mkuu (Papa wa Katoliki) asubuhi ya Jumamosi mwezi (21 Rajabu 1442h) sawa na tarehe (6 Machi 2021m), lifuatalo ni tamko kuhusu swala hilo:
Ni matumaini yetu viongozi wakuu wa Dini na kiroho watumie akili na kuacha kutumia lugha za vita na kuweka mbele maslahi binafsi badala ya haki ya kuishi kwa uhuru na utulivu, akasisitiza umuhimu wa kuongeza juhudi ya kulingania maelewano na kuishi kwa amani na ushirikiano katika jamii, akahimiza kuheshimu haki za watu na kuheshimiana kwa watu wanao tofautiana Dini milengo na fikra.