Vikao vya uwasilishaji wa mada za kitafiti katika kongamano la kuchomoza kwa miezi ya elimu

Maoni katika picha
Alasiri ya Alkhamisi mwezi (4 Shabani 1442h) sawa na tarehe (18 Machi 2021m) vimeanza vikao vya uwasilishaji wa mada za kitafiti katika kongamano la kuzaliwa miezi ya Muhammadiyya chini ya anuani isemayo: (Kuchomoza miezi.. uhuishaji wa mwenendo wa Mtume mteule na Aali zake watakatifu), na kauli mbiu isemayo: (Harakati za kielimu kati ya Madina na Karbala), linalo simamiwa na jumuiya ya Al-Ameed kwa kushirikiana na muwakilishi wa Atabatu Abbasiyya katika nchi za Ulaya na chuo kikuu cha kiislamu cha Lebanon.

Kikao cha uwasilishaji wa mada za kitafiti kimeongozwa na Dokta Ali Mislawi, alifundua kwa kushukuru ushiriki wa watafiti katika kongamano hili, sambamba na kuishukuru Atabatu Abbasiyya tukufu kwa ulezi wake katika harakati hii.

Mada zilizo wasilishwa ni:

  • - Mada ya kwanza: (Kujitolea na siri ya utendaji kwa Ahlulbait –a.s-) imewasilishwa na Dokta Muhammad Abdallah/ kutoka chuo kikuu cha kiislamu cha Lebanon.
  • - Mada ya pili: (Mwenendo wa Imamu Sajjaad na mwanae Baaqir –a.s- katika malezi na elimu) imewasilishwa na Dokta Karim Hussein Naaswihi/ kutoka jumuiya ya kielimu Al-Ameed.
  • - Mada ya tatu: (Abbasi –a.s- mfundishaji wa ubunifu na elimu) imewasilishwa na Dokta Shekh Mahadi Gharuwi/ kutoka chuo kikuu cha kiislamu cha Lebanon.
  • - Mada ya nne: (Athari ya kuzaliwa miezi mitatu katika masomo ya kihistoria na kijamii) imewasilishwa na Dokta Daudi Zubaidi/ kutoka chuo kikuu cha Al-Ameed.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: