Maneno ya ukaribisho yanasikika katika minara ya malalo mbili takatifu

Maoni katika picha
Maneno ya kukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhani, mwezi wa rehema, maghafira na ibada, utakao anza kesho siku ya Jumatano tarehe (14 Aprili 2021m), yanasikika katika malalo mbili takatifu ya Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s) kabla ya adhana ya Magharibi.

Miongoni mwa maneno hayo ni:

Karibu karibu karibu

Karibu ewe mwezi wa Ramadhani

Karibu ewe mwezi wa kukombolewa na moto karibu

Karibu ewe mwezi wa twaa na msamaha

Karibu ewe mwezi wa wema na ihsaan

Karibu karibu karibu

Karibu elfu moja kwa kipenzi mwema baina ya walimwengu

Karibu elfu moja kwa mliwazaji wa kudumu kwa walimwengu

Ewe muokozi wa watu sisi tunaogelea katika giza…

Ukaribisho huo ni kitendo cha kurithi, kimekuwa kikifanywa kila unapokaribia kuingia mwezi mtukufu wa Ramadhani, watu wa Karbala wamezowea kusikia ukaribisho huo kana tangazo la kuanza kwa funga, katika zama hizi umekua ukitolewa kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, wasomaji wa Ataba mbili takatifu husoma tenzi na kaswida nzuri zinazo andaa nyoyo za waumini, waliopo katika malalo mbili takatifu ya Abu Abdillahi Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s), au katika uwanja wa katikati ya haram mbili tukufu na maeneo yanayo zunguka sehemu hiyo, au wale wanao angalia katika luninga zao.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: