App ya marafiki wa maktaba ya Ummul-Banina ya wanawake

Maoni katika picha
Ofisi ya Ummul-Banina (a.s) ya wanawake chini ya kitengo cha habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya imeandaa App maalum iitwayo (marafiki wa maktaba), kwa ajili ya kuongeza mawasiliano na wadau wake na kupanua wigo wa huduma, na kutumia teknolojia za kisasa kwa usahihi, App hiyo itasaidia toghuti rasmi ya maktaba na kumrahisishia mtumiaji kunufaika na huduma zinazo tolewa na maktaba.

Mkuu wa maktaba bibi Asmahani Raádu amesema: “App imetengenezwa na kupangiliwa kisasa na rahisi kuitumia, mtumiaji anaweza kufungua kwa urahisi na kufaidika na huduma zinazo tolewa ikiwa ni pamoja na kufungua vitabu na kujisomea”.

Akaongeza kuwa: “App inasifa zifuatazo:

  • Imesanifiwa vizuri na inavutia ni rahisi kuitumiwa na kila mtu.
  • Inapicha nyingi za mnato na video za wasomaji wengi.
  • Imepangiliwa vizuri katika ukurasa wake mkuu.
  • Unaweza kushiriki katika shindano la marafiki wa maktaba kwa kusoma vitabu vingi zaidi.
  • Inaingiza vitabu vipya kila wakati.
  • Inafuatilia mashindano pamoja na huduma zinazo tolewa na maktaba.
  • Ushirikiano wa wazi na mzuri”.

Akaendelea kusema: “App kwa sasa inapatikana kwenye vifaa vyenye (Android) na juhudi zinafanyika ipatikane kwenye vifaa vyenye (ios) pia”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: