Wito wa kushiriki kwenye semina ya fani za uongeaji

Maoni katika picha
Jumuiya ya Skaut Alkafeel chini ya idara ya watoto wa makuzi katika kitengo cha Habari cha Atabatu Abbasiyya tukufu, imekusudia kutoa mafunzo ya fani za uongeaji katika program ya kujenga uwezo awamu ya tano, inamkaribisha kila anayehisi anaweza kuongea (kutoa mhadhara) mbele za watu, ajisajili kupitia telegram kwa link ifuatayo @Rhusdsn.

Mafunzo haya yanalenga kujenga uwezo wa vijana na kuendeleza vipaji vyao, wakufunzi ni wasomi waliobobea katika fani hiyo, watafundishwa mambo mbalimbali yanayo endana na umri wa washiriki ambao ni miaka (10 – 18).

Mada zitakazo fundishwa ni:

  • - Kujiamini na uthubutu.
  • - Mahadhi ya sauti.
  • - Mahadhi ya lugha ya muili.

Aidha semina itakua na masomo ya Akhlaqi, Aqida na mengineyo, watafundishwa kwa nadhariyya na vitendo, vile vile kutakua na mijadala pamoja na majaribio, mwisho wa semina washiriki wote watapewa vyeti vya ushiriki na zawadi kwa watakao fanya vizuri.

Watakao faulu watapewa kipaombele cha kushiriki katika semina zingine na kuendeleza vipaji vyao ili kutengeneza kizazi cha wahadhiri bora.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: