Toleo la ishirini na mbili la jarida la (Al-Aqiida)

Maoni katika picha
Hivi karibuni kituo cha kiislamu cha masomo ya kimkakati chini ya kitengo cha Habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya kimechapisha toleo la ishirini na mbili la jarida la (Al-Aqiida).

Toleo hili linamada nyingi, miongoni mwa mada zake ni:

  • - Fatuma Zaharaa (a.s) na nusra ya uislamu muhammadiyya/ Dokta Aamir Abduzaid Al-Waailiy.
  • - Mazingatio katika kubainisha uwelewa wa kusubiri/ Mheshimiwa Sayyid Mahmuud Almuqaddasi Algharifi.
  • - Turathi za kiaqida kwa Shia Imamiyya (utafiti wa Babaliyughurafiyya) kuanzia kwa Shekhe Swaduuq hadi kwa Allamah Hilliy.
  • - Riwaya ya (Soma.. mimi sio msomaji) ni wahyi au uzushi?!/ Dokta Kaadhim Nasru-Llah.
  • - Njia za kurekebisha jamii ya kiislamu kutokana na fikra za chuki za kisasa katika mtazamo wa Sayyid Shahidi Muhammad Baaqir, utafiti wa kidalili/ Dokta Baasim Abdulhussein Raahi Alhasanawi/ katoa nakala na mifano halisi.
  • - Ubatili wa misingi ya falsafa ya kimagharibi katika mtazamo wa mitafizikia kwa watawala wa kwanza wa kiyunani/ Dokta Sanusi Saami.

Kumbuka kuwa jarida la (Al-Aqiida) ni miongoni mwa majarida yanayo tolewa na kituo, nalo huandika mambo ya Aqida na (Ilmu-Kalaam) ya zamani na sasa, kwa kuzingatia hoja za kiakili na dalili kutoka katika vizito viwili.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: