Maahadi ya Qur’ani tukufu tawi la Hindiyya chini ya Atabatu Abbasiyya, inatoa masomo kwa wanafunzi wanaoshiriki kwenye semina ya Baswairul-Qur’aniyyah kwa njia ya mtandao, masomo wanayo fundishwa ni (hukumu za usomaji, kuhifadhi na maarifa ya Qur’ani tukufu) washiriki wapo wanafunzi (100) kutoka mikoa tofauti ya Iraq.
Semina hii inatokana na juhudi za tawi la Maahadi za kuendelea kufundisha Qur’ani tukufu na kutumia faragha za wanafunzi.
Kumbuka kuwa Maahadi ya Qur’ani kupitia matawi yake yote, inaendesha miradi na kufanya harakati mbalimbali za ufundishaji wa Qur’ani, kwa ajili ya kuwafanya vijana wakitambue kitabu cha Mwenyezi Mungu na kukihifadhi, imekua ikitoa elimu kwa kutumia njia tofaoti zikiwemo na teknolojia za kisasa.