Idara ya Qur’ani inaendesha mashindano ya kuhifadhi khutuba ya bibi Zainabu (a.s)

Maoni katika picha
Idara ya Qur’ani inaendesha shindano la kuhifadhi khutuba mashuhuri ya bibi Zainabu (a.s) aliyotoa katika majlisi ya Yazidi.

Kiongozi wa Idara hiyo bibi Fatuma Sayyid Abbasi Mussawi amesema: “Kutokana na ukubwa wa jambo hili tumeruhusu ushiriki wa wanawake wa rika zote, majina ya washindi yatatangazwa mwezi wa Rabiul-Awwal kupitia mtandao wa idara ya Qur’ani wa facebook”.

Akasema: “Ushiriki wa shindano hili unafanywa kwa kujisajili kupitia anuani (alwahdaalqurania@) na mshiriki ataje taarifa zifuatazo: (Majina matatu, umri, mkoa, namba ya simu, kiwango cha elimu yake)”, akaongeza kuwa: “Baada ya hapo atapigiwa simu ya video na wakina dada wanao simamia shindano hilo na kusoma moja kwa moja khutuba hiyo”.

Akakumbusha kuwa: “Wataanza kupigiwa simu mwezi (21 Safar) hadi mwisho wa mwezi, khuduba ihifadhiwe kama ilivyo andikwa katika kitabu cha (Luhuufu fii qatla tufuuf)”, akasema kuwa: “Kutakua na zawadi kwa washindi wa shindano hili”.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na idara kupitia ukurasa wake wa facebook.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: