Kurefusha muda wa kupokea nyaraka za washiriki wa shindano la (dondoo za ujumbe wa wapenzi wa Husseini)

Maoni katika picha
Idara ya kusaidia wasomaji wa Qur’ani chini ya maktaba ya Ummul-Banina (a.s) tawi la wanawake katika Atabatu Abbasiyya tukufu, imetangaza kuongeza muda wa kupokea nyaraka za ushiriki wa shindano la (dondoo za ujumbe wa wapenzi wa Husseini) la wanawake, hadi siku ya Alkhamisi mwezi (29 Safar 1443h) sawa na tarehe (7 Oktoba 2021m), ili kutoa nafasi zaidi kwa washiriki baada ya kumaliza ziara ya Arubaini, nyaraka za ushiriki zitumwe kupitia barua pepe ifuatayo: readingandreceivingunit@gmail.com au kwa telegram kupitia namba ya simu (07602363311).

Shindano linahusisha vipande vya video vilivyo rekodiwa mambo yanayo endana na utamaduni wa Husseiniyya yanayo onyesha matendo ya kibinaadamu na kiislamu katika matembezi ya Arubaini chini ya mada zifuatazo:

  • Usafi na muonekano wa utamaduni wa Husseiniyya.
  • Kazi za kujitolea na kusaidiana kijamii.
  • Hijabu na utamaduni wa Zainabiyya.
  • Picha ya malezi ya Husseiniyya katika mwenyendo wa watoto.
  • Muonekano wa kulinda neema na kutofanya ubadhirifu.

Chini ya kanuni zifuatazo:

  • Kipande cha video kisizidi dakika tatu.
  • Unaweza kuandaa video na kuipeleka kwenye kamati inayohusika na video.
  • Muonekano wa picha usiwe chini ya 1mb, hakikisha video inamuonekano mzuri.
  • Isiwe na nembo yeyote au alama ya kibiashara.
  • Picha zisiwekwe kitu chochote, kama maandishi, nembo na alama.

Masharti ya shindano:

  • Mshiriki anahaki ya kutuma picha moja au mbili.
  • Mshiriki haruhusiwi kutuma video zaidi ya moja.
  • Video iwe haijawahi kuonekana sehemu nyingine, au kushiriki kwenye shindano lingine.
  • Maktaba inahaki ya kutumia itakavyo.
  • Mshiriki anahaki ya kunufaika na kazi yake katika upande wa usanifu, kwenye majarida na sehemu zingine.
  • Kazi zote zitawasilishwa kwenye kamati ya majaji watakao chuja na kupata washindi watano upande wa sauti na watano upande wa video.
  • Kazi hizo zitawekwa kwenye mtandao maalum wa maktaba.
  • Majina ya washindi yatatangazwa mwezi (9 Ribiul-Awwal 1443h) sawa na tarehe (16 Oktoba 2021m).
  • Washindi watano wa mwanzo katika kila kipengele watapewa zawadi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: