Atabatu Abbasiyya tukufu kupitia shamba boy wake, inapanda miti kwenye shule za hapa Karbala, chini ya mradi wa kupanda miti mjini ulioanza tangu mwaka (2011) na bado unaendelea hadi sasa.
Mradi huu ni sehemu ya kuweka kijani kibichi kwa bupanda miti inayo endana na mazingira ya hali ya hewa ya Iraq.
Kazi ya kupanda miti itahusisha shule za mkoa wa Karbala kwa kupanda miti ya aina tofauti, kitengo kimeotesha miti kwa wingi, tambua kuwa miti inayopandwa ni:
Senne surattensis
Acacia saligna
Callistemon viminalis
Brachychiton acerifolius
Moringa oleifera
Bombax ceiba
Jacaranda mimosifolia
Delonix regia
Albizia lebbeck
Terminalia ivorensis
Eucalyptus spp
Ziziphus spina
Olea spp
Citrus aurantium
Viongozi wa shamba boy wanatoa wito kwa wakuu wa shule na walimu kuleta maombi ya kupandiwa miti katika shule zao, kwa kujaza fomu maalum iliyoandaliwa na shamba boy wa Alkafeel.
Tambua kuwa maombi yanapokelewa kuanzia saa moja asubuhi hadi saa nane baada ya Adhuhuri, tunaendelea kupokea maombi hadi siku ya Jumapili tarehe (24 Oktoba 2021m), tutaandaa miti na kuja kupanda bure..
Mambo yanayo hitajika kwa muombaji ni:
Kujaza fomu.
Kitambulisho cha taifa au cha kazi.