Kikao cha mwisho kimeorodhesha maazimio yaliyo tolewa na washiriki wa kongamano hilo, yamesomwa na rais wa kitengo cha Habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya Ustadh Aqiil Abdulhusein Alyaasiriy, kama ifuatavyo:
- 1- Umuhimu wa kushirikiana baina ya serikali na vituo vya tafiti vinavyo husika na kuthibitisha jinai na vitendo vya ugaudi, ili kurahisisha utendaji wao.
- 2- Kuvipa nafasi vyuo vikuu vya Iraq ya kuthibitisha jinai na vitendo vya ugaidi vilivyo vyanywa Iraq, kwa kuandika vitabu na tafiti za kielimu sambamba na kufanya nadwa, warsha na makongamano.
- 3- Kuunda kamati itakayo jumuisha wajumbe kutoka wizarati na kwenye taasisi za kiraia pamoja na vituo vinavyo fanya kazi ya kuthibitisha jinai na vitendo vya ugaidi.
- 4- Kufanya kongamano maalum la kitaifa kwa ajili ya kuthibitisha jinai na vitendo vya kigaidi.
- 5- Kufanya mashindano ya kitabu bora cha kuthibitisha jinai na vitendo vya kigaidi, na mashindano ya filamu bora, na picha bora na bango bora.
- 6- Kongamano hili lifanywe kila mwaka sambamba na matukio ya kielimu.
Mwisho washiriki wa kongamano wakapewa zawadi.