Hatua za mwisho za maandalizi ya hafla ya kuhitimisha maswala ya malezi

Maoni katika picha
Watumishi wa kitengo cha malezi na elimu ya juu katika Atabatu Abbasiyya tukufu, wanafanya maandalizi ya mwisho ya hafla ya kuhitimisha maswala ya malezi, katika shule za awali za Al-Ameed, itakayo fanyika kesho asubuhi.

Rais wa kitengo hicho Dokta Ahmadi Swabihi Kaabi amesema: “Shule za Al-Ameed hufanya hafla kubwa kila mwaka inayohusu maswala ya malezi kwa wanafunzi wake wa awali, kupitia program ya (Nahwul-Qamaru)”.

Akaongeza kuwa: “Watoto watafanya mambo mbalimbali waliyo fundishwa ikiwa ni pamoja na maigizo katika kuonyesha wazazi wao kuwa wako tayali kuingia shule ya msingi”.

Akaendelea kusema: “Program ya (Nahwul-Qamaru) ni program ya kielimu na kimalezi iliyo andaliwa rasmi kwa shule za awali za Al-Ameed, inahusu mambo mengi yanayofundishwa kwa watoto hao, malezi, Dini, utamaduni na mambo mengine yatakayo wasaidia katika maisha yao ya baadae”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: