Atabatu Abbasiyya tukufu inatoa pongezi kwa Imamu wa zama, Imamu Mahadi msubiriwa (a.f), na Maraajii watkufu pamoja na waislamu wote kwa kufikiwa na Idul-Ghadiir, siku ya kutimia neema na kukamilika Dini na kutawazwa kwa Imamu Ali bun Abu Twalib (a.s).
Tunamuomba Mwenyezi Mungu mtukufu atujaalie kuwa katika wenye kushikamana na uongozi wake, atuweke pamoja na kiongozi wa waumini (a.s), arudishe siku hii kwa waislamu wote wakiwa wenye afya na amani, alipe taifa letu neema ya amani na utulivu.