Kumtambua.. Shindano la kimtandao lenye anuani isemayo (Utafiti katika turathi za Sayyid Muhammad Saidi Alhakiim).

Kitengo cha Habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya tukufu, kinafanya shindano kwa njia ya mtandao lenye anuani isemayo (Utafiti katika turathi za Sayyid Muhammad Saidi Alhakiim).

Shindano hilo linasimamiwa na Maahadi ya turathi za mitume na tafiti za kihauza chini ya kitengo.

Shindano linahusu vitabu vitatu vilivyo andikwa na Sayyid Alhakiim, ambavyo ni:

  • 1- Khatamu-Nnabiyyina.
  • 2- Usulul-Aqidah.
  • 3- Faajiatu-Twafu.

Washindi wanne wa kwanza watapewa zawadi zifuatazo:

  • 1- Mshindi wa kwanza: Atapelekwa kufanya Umra.
  • 2- Mshindi wa pili: Atapelekwa kufanya ziara kwa Imamu Ridhaa (a.s).
  • 3- Mshindi wa tatu: Atapewa kompyuta yenye thamani ya (dola 400).
  • 4- Mshindi wa nne: Atapewa riyali laki moja na vitabu vya Maahadi.

Shindao litadumu kwa muda wa miezi mitatu, kuanzia mwezi wa Rabiul-Aakhar, matokeo yatatangazwa mwezi kumi na tano Shabani mwaka huu wa 1444h.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: