Balozi wa Uturuki nchini Iraq ametembelea Atabatu Abbasiyya na kujadili namna ya kushirikiana na kusaidiana

Baada ya Adhuhuri ya siku ya Alkhamisi mheshimiwa Balozi wa Uturuki nchini Iraq Ali Ridha Kunai, ametembelea Atabatu Abbasiyya tukufu.

Amepokewa na katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya Sayyid Mustwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini na viongozi wengine wa Ataba.

Wamejadili njia za kusaidiana na kushirikiana kati ya Atabatu Abbasiyya na Uturuki, hususan upande wa biashara.

Katika kikao hicho Atabatu Abbasiyya imeeleza baadhi ya miradi yake na mafanikio yaliyopatikana.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: