Mheshimiwa kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya Sayyid Ahmadi Swafi, amesisitiza kuwa kufanya kazi chini ya Abulfadhil Abbasi (a.s) ni neema kutoka kwa Mwenyezi Mungu mtukufu, yapasa kushukuru.
Mheshimiwa kiongozi mkuu wa kisheria ametoa nasaha muhimu kwa viongozi wa idara kuhusu changamato za kazi, sambamba na kuwapa muongozo wa utendaji wa majukumu yao.
Miongoni mwa mambo aliyo sisitiza ni umuhimu wa kutenga muda wa kutumikia sehemu hii takatifu, sambamba na kutafakari namna ya kuendeleza taasisi hii tukufu.
Mheshimiwa ameendelea kusisitiza umuhimu wa kutenga muda wa kufanya kazi na kufanya ibada, pamoja na kuchukua mazingatio katika historia za Ahlulbait (a.s).