Kitengo cha usimamizi wa haram kinatoa huduma mbalimbali kwa mazuwaru katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Kitengo kinachosimamia haram tukufu katika Atabatu Abbasiyya, kinatoa huduma mbalimbali kwa mazuwaru toka siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Sayyid Ali Muhammad amesema “Miongoni mwa kazi tunazofanya ni kudumisha usafi katika haram tukufu, kupuliza marashi, kuweka idadi kubwa ya misahafu, vitabu vya dua na ziara pamoja na turba za kutosha”.

Akaongeza kuwa “Miongoni mwa majukumu ya kitengo kinachosimamia haram, ni kuongoza utembeaji wa mazuwaru ndani ya haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s), na kuandaa sehemu za kuswalia”.

Kwa mujibu wa maelezo ya Muhammad “Watumishi wa kitengo hiki wanakazi nyingi, miongoni mwa kazi zao, ni kufanya usafi muda wote na kubadilisha mazulia kila inapohijatika”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: