Msahafu wa tunda la Arubaini umepata muitikio mkubwa katika tawi la Majmaa-Ilmi kwenye maonyesho ya Tehran.

Machapisho ya Majmaa-Ilmi ya Qur’ani tukufu katika Atabatu Abbasiyya, ukiwemo msahafu wa tunda la Arubaini, ulioandikwa kwa mikono ya mazuwaru umevutia watu wengi kwenye maonyesho ya kimataifa yanayofanyika Tehran.

Katika machapisho yaliyovutia watu wengi ni misahafu iliyo chapishwa na Majmaa, kulikuwa na aina sita za misahafu yenye ukubwa tofauti, iliyoandikwa kwa hati za kiiraq na kuwekwa mapambo ya kiiraq, misahafu hiyo ilichapishwa na kituo cha uchapaji cha Atabatu Abbasiyya.

Machapisho ya Qur’ani kutoka Atabatu Abbasiyya tukufu yamepata heshima maalum kwenye maonyesho ya kimataifa ya thelathini nchini Iran, yametembelewa na watu wengi sana wakiwemo viongozi wa kidini na kijamii.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: