Matembezi ya maukibu yameanzia ndani ya haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s), wakapitia uwanja wa katikati ya haram mbili huku wanaimba kaswida za kuomboleza zilizo amsha hisia ya huzuni katika nyoyo za waumini na wapenzi wa Ahlulbait (a.s).
Baada ya kuwasili katika haram ya Imamu Hussein (a.s) wakafanya majlisi ya kuomboleza kwa ushiriki wa mazuwaru wengi, hapo zikasomwa tenzi na kaswida zilizoeleza maisha na historia ya Imamu Ali (a.s).