Kitengo cha utumishi kinafanya usafi katika maeneo yote yanayozunguka Atabatu Abbasiyya.

Kitengo cha usafi katika Atabatu Abbasiyya tukufu kimeanza kazi ya kusafisha jengo tukufu la malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) na maeneo yote yanayozunguka jengo hilo takatifu.

Makamo rais wa kitengo hicho Mhandisi Abbasi Ali amesema “Baada ya kimbunga na mvua ya jana siku ya Jumatano, watumishi wetu leo asubuhi wameanza kazi ya kusafisha jengo takatifu na maeneo yeto yanayozunguka malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s)”.

Akaongeza kuwa “Kazi ya usafi imehusisha barabara zinazozunguka malalo takatifu”.

Akafafanua kuwa “Wahudumu wetu walianza kusafisha eneo la mlango wa Qibla kwa kutumia vifaa mbalimbali, wakaendelea kusafisha na maeneo mengine”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: