Rais wa kitengo cha mgahawa Sayyid Aadil Jafari amesema “Idadi ya mazuwaru inaongezeka kila siku katika mji wa Karbala ndani ya siku hizi la Lailatul-Qadri, watu wanakuja kumtembelea Imamu Hussein na ndugu yake Abulafadhil Abbasi (a.s), jambo hilo linasababisha na sisi kuongeza huduma katika mgahawa (mudhifu) wetu.
Akaongeza kuwa: “Ndani ya siku tatu za Lailatul-Qadri, mgahawa umegawa zaidi ya sahani za chakula (150,000) sambamba na ugawaji wa maji ya kunywa, juisi, matunda na vitafunwa”.
Mgahawa wa Atabatu Abbasiyya hutoa huduma bora kwa mazuwaru wanaokuja kumtembelea Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s) mwaka mzima.