Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya anatembelea kitengo cha shughuli za idara na kuangalia utendaji wao.

Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya Sayyid Ahmadi Swafi siku ya Ijumaa, ametembelea kitengo cha shughuli za idara na kuangalia utendaji kazi wao.

Rais wa kitengo Sayyid Riyaadh Hamza Ahmadi amesema “Leo tumetembelewa na kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya Mheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi na katibu mkuu Sayyid Mustwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini pamoja na wajumbe wa kamati kuu, wameangalia utendaji wetu wa kazi”.

Akaongeza kuwa “Mheshimiwa ameangalia utendaji kazi wa rasilimali watu kwa njia ya mtandao, kuanzia makazi, ruhusa, adhabu, mapumziko na mambo mengine yanayohusiana na watumishi wa Ataba tukufu”.

Akasisitiza kuwa “Mheshimiwa na wageni aliofuatana nao, wamepongeza utendaji wa kazi katika idara yetu na utaratibu unaotumika”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: