Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya anapokea watu wanaokuja kutoa salam za Idhul-Adh-ha.

Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya Mheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi, asubuhi ya Alkhamisi amepokea watu wanaokuja kutoa salam za Idhul-Adh-ha.

Katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya Sayyid Mustwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini na wajumbe wa kamati kuu pamoja na marais wa vitengo, wameshiriki katika kupokea wageni na salam za Idi.

Viongozi mbalimbali wa mkoa wa Karbala wamekuja Atabatu Abbasiyya kutoa salam za Idhul-Adha-ha.

Katika kubadilishana salam za Idi wahudumu wa malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) wamemuomba Mwenyezi Mungu mtukufu, arudishe tukio hili mwakani huku taifa likiwa na amani na utulivu.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: