Watumishi wa kitengo kinachosimamia uwanja wa katikati ya haram mbili wamevuna tende zilizopo kwenye eneo hiyo takatifu.

Watumishi wanaohudumia uwanja wa katikati ya haram mbili tukufu, wamevuna tende zilizopo katika eneo la katikati ya malalo ya Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s).

Kiongozi wa idara ya miti na mapambo amesema “Watumishi wetu wamevuna tende zilizopo kwenye uwanja wa katikati ya Ataba mbili ya Husseiniyya na Abbasiyya”.

Akaongeza kuwa “Eneo la katikati ya haram mbili linamitende (56) ambayo ni sawa na umri wa Imamu Hussein (a.s), tende hizo huvunwa kila mwaka na kuzigawa kwa mazuwaru wa bwana wa mashahidi na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s) kwa tabaruku.

Kitengo kinachosimamia uwanja wa katikati ya haram mbili kinajukumu la kutunza miti iliyopo eneo hilo takatifu, hususa mitende na kuvuna matunda yake.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: