Jumuiya ya Skaut ya Alkafeel chini ya kitengo cha Habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya tukufu, imeadhimisha mazazi ya Imamu Mahadi (a.f).
Hafla imefunguliwa kwa Qur’ani tukufu, iliyofuatiwa na muhadhara kuhusu kumsubiri Imamu Mahadi (a.f) kutoka kwa Shekhe Ahmadi Al-Aamiliy, muongoza kikao alikuwa ni kiongozi wa Skaut Amiri Kaadhim.
Hafla imepambwa na tenzi zilizoamsha hisia za furaha kufuatia tukio hilo tukufu na ikahitimishwa kwa kugawa zawadi kwa washiriki wote.