Chuo kikuu cha Alkafeel kimefanya kikao cha kujadili maandalizi ya mtihani wa mwisho wa mwaka wa masomo 2024m.
Kikao hicho kimeandaliwa na baraza la chuo kwa lengo la kujadili maandalizi ya mtihani wa mwisho wa muhula wa masomo.
Kikao kimeongozwa na mkuu wa chuo Dokta Fadhili Ismaili Sharadi na kuhudhuriwa na wajumbe wa kamati ya walimu, wamejadili mambo mengi ikiwa ni pamoja na ratiba ya mitihani.
Aidha kikao hicho kimejadili mambo tofauti kuhusu sekta ya elimu na kujenga ushirikiano endelevu kwa ajili ya kuwa na matokeo bora ya elimu.