Idara ya Fatuma binti Asadi ya masomo ya Qur’ani imefanya hafla ya wahitimu wake wa kwanza.

Idara ya Fatuma binti Asadi (a.s) ya masomo ya Qur’ani katika Atabatu Abbasiyya tukufu, imefanya hafla ya wahitimu wake wa kwanza.

Kiongozi wa idara bibi Fatuma Mussawi amesema “Idara ya Fatuma binti Asadi ya masomo ya Qur’ani imefanya hafla ya wahitimu wake wa kwanza, waliosoma kwa muda wa miaka (6), miongoni mwa mada walizofundishwa ni (Nahau, Fiqhi, Aqida, Ulumul-Qur’ani, Balagha na hukumu za usomaji wa Qur’ani).

Akaongeza kuwa “Idara inazingatia na kutilia uhuminu sana harakati na miradi inayohusu Qur’ani tukufu”

Mwanafunzi Majidah Hussein Jaasim amesema “Atabatu Abbasiyya tukufu kuandaa hafla ya wahitimu ni jambo zuri, hatuna la kusema zaidi ya kushukuru idara ya Ataba tukufu chini ya kiongozi mkuu wa kisheria Sayyid Ahmadi Swafi na viongozi wa idara ya Fatuma binti Asadi ya masomo ya Qur’ani kwa kazi kubwa waliyofanya ya kufanikisha ratiba hii”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: