Katika kuadhimisha mazazi ya Imamu Ridhwa (a.s).. mashada ya mauwa yamepamba dirisha la malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s).

Idara ya haram tukufu katika Atabatu Abbasiyya imeweka mauwa kwenye dirisha la malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) katika kuadhimisha mazazi ya Imamu Ridhwa (a.s).

Watumishi wa idara wamezowea kuhuisha matukio ya Ahlulbait (a.s), likiwemo la kuzaliwa Imamu Ridhwa (a.s).

Kazi ya upambaji wa dirisha imehusisha kuweka mauwa yenye rangi tofauti na harufu nzuri, kwa lengo la kuongeza uzuri juu ya uzuri kwenye malalo ya mwezi wa bani Hashim (a.s).

Atabatu Abbasiyya huweka mapambo yanayoashiria furaha juu ya dirisha la kaburi takatifu katika kuadhimisha mazazi ya watakasifu miongoni mwa watu wa nyumba ya Mtume (a.s).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: