Kitengo cha Maqaam kimejipanga kupokea mazuwaru wa siku ya Arafa na Idul-adh-ha

Kitengo cha Maqaam ya Imamu Hujjah (a.s) chini ya Atabatu Abbasiyya kimejiandaa kupokea mazuwaru wa siku ya Arafa na Idul-adh-ha.

Makamo rais wa kitengo Sayyid Hadi Mahdi Muhammad amesema “Watumishi wetu wamejiandaa kupokea mazuwaru wa siku ya Arafa na Idul-adh-ha”, akasema “Tumeandaa sehemu maalum kwa ajili ya swala na dua”.

Akaongeza kuwa “Maandalizi yamehusisha uwekaji wa maji safi ya kunywa, juisi na gari maalum za kubeba taka”.

Kitengo hutoa huduma zinazorahisisha ufanyaji wa ziara na ibada zingine.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: