Katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya anaangalia mahitaji ya mawakibu za kutoa huduma.

Katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya Sayyid Mustwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini, anaandalia mahitaji ya mawakibu za kutoa huduma zilizopo karibu na Ataba tukufu.

Jambo hilo analifanya chini ya maelekezo ya kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya, Muheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi, kwa lengo la kurahisisha utendaji wa mawakibu na kuangalia mahitaji yao zikiwa zimebaki siku chache kuingia mwezi wa Muharam na ziara ya Ashura.

Muheshimiwa katibu mkuu amefuatana na rais wa maadhimisho na mawakibu Husseiniyya chini ya Ataba mbili tukufu Husseiniyya na Abbasiyya Sayyid Ali Muslihu na baadhi ya wawakilishi wa vitengo vya Atabatu Abbasiyya.

Ataba tukufu hufanya kila iwezalo katika kurahisisha utoaji wa huduma kwa mazuwaru wa Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s) katika mwezi wa Muharam na Safar.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: