Majmaa-Ilmi imefanya kikao cha usomaji wa Qur’ani kwa lengo la kuboresha uwelewa wa Qur’ani na kusambaza utamaduni wake

Majmaa-Ilmi ya Qur’ani tukufu katika Atabatu Abbasiyya imefanya kikao cha usomaji wa wa Qur’ani katika mtaa wa Huriyya, kwa lengo la kuboresha uwelewa na kusambaza utamaduni wake.

Kikao kimefunguliwa kwa Qur’ani tukufu iliyosomwa na Akram Saamir, yakafuata mawaidha kutoka kwa Shekhe Zainul-Aabidina Abayati, ameongea maana ya kujitolea alikofanya Imamu Hussein (a.s) na wafuasi wake.

Akaeleza umuhimu wa kukumbuka misingi ya Imamu Hussein (a.s) na kuifundisha katika nyoyo za waislamu, hususan vijana.

Kikao kimeshuhudia upandishwaji wa bendera ya Abulfadhil Abbasi (a.s), kikahitimishwa kwa Qur’ani tukufu iliyosomwa na Ahmadi Zaalimi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: