Uongozi mkuu wa Atabatu Abbasiyya umetangaza orodha ya huduma zake wakati wa ziara ya Arubaini ya Imamu Hussein (a.s) kuanzia mwezi mosi hadi ishirini Safar.
Katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya Sayyid Mustwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini amesema “Vituo vya Dini na utamaduni vilikuwa 180, jumla ya machapisho yaliyotolewa na Atabatu Abbasiyya yamefika 300,000, vituo vya vijana wa Alkafeel vimehudumia mazuwaru 39.531”.
Akaongeza kuwa “Huduma za Ataba tukufu katika sekta ya Qur’ani imefanywa kupitia vituo vya Qur’ani 100 vilivyokuwa na walimu 1140, wanufaika wa vituo hivyo wamefika mazuwaru 532,905”.
Akaendelea kusema “Ziara ya Arubaini mwaka huu imefanyika wakati wa joto kali, hivyo Atabatu Abbasiyya iliweka miundombinu ya kusaidia kupunguza joto, tulifunga kitambaa cha Saraani cha kijani kwa lengo la kupunguza joto la jua katika maeneo yanayozunguka Ataba tukufu, jumla ya mita 100.000 za kitambaa hicho zimefungwa, mita 40.000 ndani ya eneo la mji wa zamani na mita 60.000 nje ya eneo hilo, tumetumia feni za kunyunyiza mazi 275, mitambo ya kusukuma maji 20”.
Kutokana na ongezeko kubwa la mazuwaru, uwanja wa Ummul-Banina (a.s), uliopo upande wa mashariki ya malalo takatifu, wenye ukubwa wa mita za mraba elfu 20 umeanza kutumika wakati wa ziara ya Arubaini na ulitengwa maalum kwa ajili ya mazuwaru wa kike.
Kuhusu huduma za afya zilizo tolewa kwa mazuwaru, katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya amesema “Tulikuwa na vituo vya afya 35, watoa huduma za dharura walikuwa 65 katika gari 30 za wagonjwa, jumla ya matukio 4112 ya uokozi yamefanyika, wanufaika wa huduma ya afya wamefika 4.045.441, miongoni mwao 80 wamepewa dawa za saratani, jumla ya tani 84.5 za dawa zimetolewa”.
Kuhusu sekta ya usafiri amesema kuwa gari 1600 zimeshiriki kubeba mazuwaru, kuhusu setka ya usafi amesema kuwa, vitengo vya Atabatu Abbasiyya tukufu vimetoa tani 4.161 za taka kuanzia mwezi mosi hadi 18 Safar.
Kuhusu sekta ya habari amefafanua kuwa “Chanel zilizorusha matangazo mubashara zilifika 123, jumla ya vitambulisho 539 vimetolewa kwa waandishi wa habari”.
Akabainisha kuwa “Jumla ya wahudumu wa kujitolea wakiwemo wa kikosi cha Abbasi (a.s), wanawake kwa wanaume imefika 22.713 katika maeneo mbalimbali yaliyochini ya Atabatu Abbasiyya”.
Kuhusu mawakibu Husseiniyya amesema kuwa, “Idadi yake imefika 13.084 za utoaji wa huduma na uombolezaji, miongoni mwake maukibu 250 za kigeni”.
Akasema kuwa vituo vya kuongoza mazuwaru vilikuwa 46 jumla ya mazuwaru 10.656 wamehudumiwa, vitambulisho vya utambuzi 144.000 vimetolewa kwa watoto na wazee, vituo vya kutunza mabegi vilikuwa 16.
Kuhusu huduma ya ugawaji wa chakula na vinywaji amesema “Atabatu Abbasiyya imegawa jumla ya sahani za chakula 10.812.984 kupitia vituo 17, hali kadhalika imegawa zaidi ya chupa za maji 64.654.080, imegawa mifuko ya barafu 235.583 na mapande ya barafu 143.464”.
Katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya ametoa shukrani nyingi kwa kila mtu aliyechangia kufanikisha ziara ya Arubaini kwa kuhudumia mazuwaru watukufu, akasisitiza kuwa wahudumu wa Atabatu Abbasiyya wanaendelea kutoa huduma kwa mazuwaru.