Wito wa kuhudhuria kongamano la kielimu la vijana

Jumuiya ya Al-Ameed na kituo cha Multaqal-Qamar chini ya kitengo cha habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya, zimetoa wito wa kuhudhuria kwenye kongamano la kielimu la kitaifa kwa vijana.

Kongamano litafanywa chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu tarehe (19 – 20/12/2024m) katika ukumbi wa Imamu Hassan (a.s) ndani ya Ataba tukufu.

Siku ya kwanza: kongamano litaanza saa saba na nusu mchana, ambapo mada nne zitawasilishwa.

Siku ya pili: litaanza saa tatu asubuhi, ambapo kutakua na maonyesho ya nasaha za Marjaa-Dini mkuu Muheshimiwa Sayyid Ali Sistani kwa vijana sambamba na kuangazia namna ya kunufaika na nasaha hizo.

Mada kuu za kongamano ni:

  • 1- Habari na mitandao ya mawasiliano ya kijamii.
  • 2- Mtazamo wa kijamii kwa Marjaiyya.
  • 3- Utambulisho wa jamii.
  • 4- Misingi ya maarifa na utamaduni.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: