Kwa ushiriki wa wanafunzi 80.. Majmaa-Ilmi imeadhimisha mazazi ya Bibi Zaharaa (a.s)

Majmaa-Ilmi ya Qur’ani tukufu katika Atabatu Abbasiyya, imeadhimisha mazazi ya Bibi Fatuma Zaharaa (a.s) katika Majmaa-Alqami kwa ushiriki wa wanafunzi 80.

Kiongozi wa idara ya habari za Qur’ani katika Maahadi Sayyid Imaad Mankushi amesema “Maahadi imeomboleza kifo cha Bibi Fatuma Zaharaa (a.s) katika Majmaa Alqami chini ya Ataba tukufu, kwa ushiriki wa zaidi ya wanafunzi 80 katika wilaya ya Husseiniyya mkoani Karbala”.

Akafafanua kuwa “Hafla imepambwa na mhadhara wa kidini ulioeleza historia ya Bibi Fatuma Zaharaa (a.s) na utukufu wake, kisha zikasomwa tenzi na qaswida”.

Akabainisha kuwa “Maahadi inalenga kujenga misingi ya kimaadili na kidini kwa wanafunzi, ili kupambana na fikra potofu zinazopandikizwa katika jamii”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: