Ujumbe huo umeongozwa na katibu mkuu wa Atabatu Husseiniyya Sayyid Hassan Abaiji, makamo wake Sayyid Muhammad Hassan Bahrul-Uluum na baadhi ya viongozi wa Ataba hiyo.
Ujumbe umepokewa na katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya Sayyid Mustwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini, makamo wake Sayyid Abbasi Mussa Ahmadi, wajumbe wa kamati kuu Sayyid Liith Mussawi, Dokta Abbasi Didah Mussawi, mkuu wa ofisi ya kiongozi mkuu wa kisheria Sayyid Jawadi Hasanawi pamoja na baadhi ya viongozi wa Ataba.
Sayyid Bahrul-Uluum amesema “Ujumbe kutoka Atabatu Husseiniyya umetoa pongezi kwa watumishi wa malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) kufuatia kuadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwake tarehe nne ya mwezi mtukufu wa Shabani”.
Akaongeza kuwa “Ujumbe umeanza matembezi yake katika malalo ya Imamu Hussein (a.s) hadi kwenye malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) wakiwa wamebeba shada za maua na kusoma maneno yanayo ashiria furaha iliyojaa katika myoyo za waumini kwa ushiriki wa kundi la mazuwaru”.













