Idara ya wahadhiri wa Husseiniyya tawi la wanawake katika Atabatu Abbasiyya imefanya hafla ya kuadhimisha mazazi ya miezi ya Muhammadiyya kwa kushirikiana na kituo cha Swidiqatu-Twahirah (a.s) katika Ataba tukufu.
Hafla imefunguliwa kwa Qur’ani iliyofuatiwa na igizo lenye anuani isemayo “Ismatul-Mu’taswimina”, limeonyesha sehemu ya maisha ya Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s).
Hafla imepambwa na shindano la Aqmaaru-Sha’baniyya, washindi wamepewa zawadi kutoka katika malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s).
Hafla ikahitimishwa kwa kusoma tenzi maalum kuhusu maadhimisho hayo matukufu.


