Kitengo cha utumishi kimeanza kukarabati kiwanda cha barafu kwa ajili ya kujiandaa na mwezi wa Muharam na Safar

Kitengo cha utumishi katika Atabatu Abbasiyya kimeanza kukarabati kiwanda cha kutengeneza barafu, ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na mwezi wa Muharam na Safar.

Kiongozi wa idara ya kitengo Sayyid Abbasi Ali amesema “Watumishi wa kitengo wamefanya ukarabati wa kiwanda cha barafu, katika sehemu ya kutengenezea na kutunzia barafu, bomba za maji (RO), ikiwa ni katika kujiandaa na msimu wa kiangazi utakaokuwa na ziara inayohudhuriwa na mamilioni ya watu, hususana katika mwezi wa Muharam na Safar”.

Akaongeza kuwa “Kiwanda cha barafu kilicho chini ya kitengo hiki, kinauweza wa kutengeneza barafu 300 kwa saa, ambazo hutolewa bure kwa mawakibu Husseiniyya na wananchi”.

Akasema kuwa “Barafu zinazobaki hutunzwa sehemu maalum, kila sehemu inauwezo wa kuingiza mifuko ya barafu 800 na kwa kiwango cha nyuzi joto 50 chini ya sifuri”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: