Wahudumu wa Atabatu Abbasiyya tukufu wanagawa pipi (halwa) kwa mazuwaru kufuatia kumbukumbu ya kuzaliwa Imamu Ridhwa (a.s)

Wahudumu wa Atabatu Abbasiyya wanagawa pipi (halwa) kwa mazuwaru kufuatia kumbukumbu ya kuzaliwa Imamu Ridhwa (a.s).

Wahudumu wa kitengo cha kusimamia haram tukufu na idara ya masayyid wameshiriki katika kugawa pipi (halwa), malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) imeshuhudia idadi kubwa ya mazuwaru waliokuja kuadhimisha tukio hilo.

Tukio hilo ni sehemu ya juhudi za Atabatu Abbasiyya tukufu, za kuimarisha mafungamano ya kiroho na kijamii kwa mazuwaru, sambamba na kuimarisha mapenzi na utiifu kwa Ahlulbait (a.s) kupitia matukio ya kidini.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: