Kitengo cha kusimamia haram kimeanza kuosha kubba ya malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) na minara yake

Wahudumu wa kitengo cha kusimamia haram katika Atabatu Abbasiyya, wameanza kuosha kubba na minara ya malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s).

Makamo rais wa kitengo Sayyid Zainul-Abidina Quraishi amesema “Wahudumu wa kitengo cha kusimamia haram tukufu wameanza kuosha kubba na minara katika malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s), ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na mwezi mtukufu wa Muharam na shughuli ya kubadili bendera, kwa kupandisha bendera nyeusi katika usiku wa kwanza wa mwezi wa Muharam”.

Akaongeza kuwa “Uoshaji unafanywa kwa umaridadi na umakini mkubwa, inatumika ngazi maalum iliyopo ndani ya Ataba tukufu, inayorahisisha kufanya kazi kwa usalama zaidi”.

Akabainisha kuwa kazi itafanywa kwa siku nne, siku mbili kuosha kubba tukufu na siku mbili zingine kuosha minara miwili, siku ya kwanza katika kila hatua itakua yakuweka ngazi, ukizingatia kuwa kazi hiyo inahitaji umakini wa hali ya juu.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: