Kubadili bendera ya kubba la malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) kufuatia kuingia mwezi mtukufu wa Muharam

Bendera nyekundu kwenye kubba la malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) imeshushwa na kupandishwa nyeusi kufuatia kuingia mwezi mtukufu wa Muharam mwaka 1447h.

Kazi ya kubadili bendera imefanywa na katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya Sayyid Mustwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini.

Wahudumu wa Ataba tukufu wameweka mabango na mapambo meusi kwenye minara na korido za haram tukufu pamoja na uzio wa nje.

Ubadilishaji wa bendera umefanywa kufuatia tangazo la ofisi ya Marjaa-Dini mkuu Ayatullahi Sayyid Husseini Sistani kuwa Ijumaa ya kesho ni siku ya kwanza ya mwezi wa Muharam (1447h).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: