Atabatu Abbasiyya imefanya majlisi ya kuomboleza katika ukumbi wa haram tukufu kufuatia kuingia mwezi wa Muharam

Atabatu Abbasiyya tukufu imefanya majlisi ya kuomboleza ndani ya ukumbi wa malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) kufuatia kuingia mwezi wa Muharam mwaka 1447h.

Mhadhiri wa Majlisi Sayyid Hishaam Albatwatwa amesema “Majlisi imefanywa saa saba mchana ndani ya ukumbi wa malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s), itadumu kwa muda wa siku kumi”, akaongeza kuwa “Wakati wa majlisi hautatizi kupita mawakibu Husseiniyya”.

Akaongeza kuwa “Majlisi zinamaudhui nyingi, miongoni mwake ni maudhui za kifikra, itikadi, maadili, malezi, historia, tukio la Ashura na Imamu Hussein (a.s), pamoja na mambo mengine mengi”.

Atabatu Abbasiyya tukufu huomboleza kumbukumbu ya Ashura na kubainisha dhulma aliyofanyiwa Imamu Hussein (a.s) na malengo ya harakati yake ya milele.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: