Kwa kuhudhuria kiongozi wake wa kisheria.. Atabatu Abbasiyya inaendelea kufanya majlisi za Husseiniyya katika mwezi wa Muharam

Uongozi mkuu wa Atabatu Abbasiyya unafanya majlisi za kuomboleza katika mwezi mtukufu wa Muharam mwaka 1447h.

Majlisi imehudhuriwa na kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya, Muheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi, katibu mkuu Sayyid Mustwafa Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini, viongozi wengine wa Ataba, wahudumu na kundi kubwa la mazuwaru na waombolezaji.

Majlisi imefunguliwa kwa Qur’ani tukufu, iliyofuatiwa na muhadhara kutoka kwa Shekhe Haazim Atwiwaani, amebainisha ulazima wa kuamrisha mema na kukataza mabaya, akasisitiza kuwa umma wa kiislamu hautakiwi kuacha jambo hilo, madam unafuata mwenendo wa Mtume Muhammad na watu wa nyumbani kwake (a.s).

Majlisi ikahitimishwa kwa kusoma tenzi na qaswida za Husseiniyya zilizo amsha hisia za huzuni na majonzi katika nyoyo za waumini.

Atabatu Abbasiyya hufanya majlisi za kuomboleza kifo cha Imamu Hussein na watu wa nyumba ya Mtume (a.s) kila mwaka.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: