Mawakibu zinaomboleza kumbukizi ya kifo cha Imamu Hassan Askariy (a.s) katika mji wa Samaraa

Mawakibu za waombolezaji zimemiminika kwa wingi katika mji wa Samaraa kutoka mikoa tofauti ya Iraq, zimekuja kuomboleza kumbukizi ya kifo cha Imamu Hassan Askariy (a.s), katika mazingira yaliyojaa huzuni kutokana na msiba huo.

Barabara za mji wa Samaraa zimejaa mawakibu za waombolezaji zikiwa na bendera zinazoashiria huzuni huku wakiimba tenzi na qaswida za uombolezaji na kuhuisha utiifu kwa Imamu mdhulumiwa.

Mawakibu za kutoa huduma mbalimbali zimejaa kwenye barabara zote zinazoelekea katika mji wa Samaraa na maeneo yanayozunguka malalo takatifu, mawakibu hizo zinagawa chakula, vinywaji na huduma zingine.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: