Wahudumu wa Atabatu Abbasiyya tukufu wamefanya tukio la kiibada katika kuomboleza kifo cha Bibi Zaharaa (a.s)

Ukumbi wa haram ya malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s), umeshuhudia tukio la kiibada lililofanywa na wahudumu wa Atabatu Abbasiyya katika kuomboleza kifo cha Bibi Fatuma Zaharaa (a.s) kwa mujibu wa riwaya ya pili.

Tukio hilo limefunguliwa kwa Qur’ani tukufu, iliyofuatiwa na usomaji wa ziara ya Abulfadhil Abbasi (a.s) kisha wimbo wa (Lahnul-Ibaa), halafu zikaimbwa qaswida na tenzi za kuomboleza zilizoeleza dhulma alizofanyiwa Bibi Fatuma Zaharaa (a.s).

Watumishi wa Atabatu Abbasiyya tukufu hufanya tukio la kiibada katika siku ya Jumatatu na Alkhamisi kila wiki.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: